A Tradition of Excellence
Kiswahili ni somo lililojengwa kumpa mwanafunzi umahiri katika myanja mbalimbali za ujifunzaji wa kusoma, kuandika , kuhesabu na kutambua tahajia na ujenzi wa umahiri katika usomaji na uandishi wa mashairi. Katika Shule ya Royal Elite yafuatayo hufanyika ili kuongeza umahiri wa matumizi ya lugha ya Kiswahili kwa wanafunzi:
  • Maigizo
  • Ngojera
  • Hadithi
  • Nyimbo
  • Kughani mashairi
  • Chemsha  bongo
Mambo hayo humfanya mwanafunzi kukuza  ufahamu na umahiri wa kuzungumza lugha ya Kiswahili. Kadhalika, humsaidia mwanafunzi kuwa na utambuzi binafsi katika utatuzi wa masuala yanayomzungaka katika mazingira yake ya kila siku katika matumizi ya lugha.